Jumamosi 5 Septemba 2026 - 08:25
Kuzingirwa Kiuchumi Kutapelekea Maadui Kushindwa

Hawza/ Ayatullah Khatami amesema: Shinikizo la kiuchumi na kuzingirwa kiuchumi vinafuatwa kwa lengo la kujenga pengo kati ya wananchi na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu na kudhoofisha kambi ya haki, lakini uzoefu wa mwanzo wa Uislamu umeonesha kwamba sera kama hizo hatimaye zitasababisha kushindwa maadui.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza kutoka Tehran, Ayatullah Sayyid Ahmad Khatami katika hotuba za Swala ya Ijumaa ya jana mjini Tehran amesema: Kila jambo tunalolifanya lina sura ya nje na undani wake, na Siku ya Kiyama undani wa mambo hayo ya nje pia utaonekana. Siku ya Kiyama ni siku ambayo mwanadamu atauona undani wa jambo alilolifanya; na kwa kuwa kafiri hakufanya jambo sahihi, atasema: “Laiti ningekuwa nimelala na nisingeyaona masiku haya.”

Aliongeza: Siku ya Kiyama si malipo pekee yatakayoonekana, bali kitendo chenyewe pia kitaonekana. Kwa hakika, hatima ya mwanadamu huko Akhera inaandaliwa na mwanadamu mwenyewe; mwanadamu mwenyewe hujijengea Pepo yake, na pia mwenyewe huitengeneza Jahannamu yake.

Imam wa muda wa Swala ya Ijumaa ya Tehran, akizungumzia shinikizo la kiuchumi na mwenendo wa Mtume wa Uislamu (saww) katika uwanja huu, alisema: Shinikizo la kiuchumi na kuzingirwa kiuchumi si jambo jipya ambalo Trump amelifanya kwa kile anachokiita sera yake; suala hili lina historia tangu mwanzo wa Uislamu.

Alikumbusha: Katika Sura Al-Anfal, aya ya 36, kuhusu wale wanaotumia mali zao katika kuipiga vita dini, imeelezwa kwamba hatimaye watajutia gharama walizotumia na watatambua kwamba hatua zao hazikutoa matokeo. Kwa hiyo, watashindwa, na huko Akhera pia watakabiliwa na mwisho mbaya.

Ayatullah Khatami alisema: Kuhusu wanafiki pia, katika Sura Al-Munafiqun, aya ya 7, imeelezwa kwamba walikuwa wakisema: “Msiwasaidie Waislamu walio pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu ili watawanyike kutoka pembeni mwa Mtume Mtukufu (saww).” Qur’ani Tukufu ni kitabu kinachozungumzia kila zama, na hii ndiyo hasa hali ya kuzingirwa kiuchumi na Marekani, ambayo inafuata malengo hayo hayo; lakini hatupaswi kusahau kwamba kama ambavyo maadui wa mwanzo wa Uislamu walishindwa, bila shaka hawa nao watashindwa.

Alisisitiza: Shinikizo la kiuchumi na kuzingirwa kiuchumi vinafuatwa kwa lengo la kujenga pengo kati ya wananchi na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu na kuidhoofisha kambi ya haki, lakini uzoefu wa mwanzo wa Uislamu umeonesha kwamba sera kama hizi hatimaye zitasababisha maadui kushindwa.

Imam wa muda wa Swala ya Ijumaa ya Tehran alisema: Mtume Mtukufu (saww) alikabiliana na shinikizo hili la kiuchumi kwa kutumia maneno mawili muhimu, akalivuka shinikizo hilo na halikuweza kumuathiri. Maneno hayo mawili muhimu bado yanahitajika kwetu leo. Neno la kwanza muhimu ni jihadi kwenye kutumia mali. Jihadi maana yake ni kujitahidi; jihadi ambayo ndani yake kuna pia ugumu na mashaka. Jihadi wakati mwingine hujitokeza katika uwanja wa kijeshi, wakati mwingine katika uwanja wa kiuchumi kwa jina la uchumi wa kujitegemea na wenye ustahimilivu, na wakati mwingine katika uwanja wa ufafanuzi kwa jina la jihadi ya ufafanuzi.

Alisisitiza kuwa: Vita vyetu vya leo ni vita mseto kwa hakika. Ni pamoja na vita vya kijeshi; vita vya kijeshi ambavyo hadi sasa vinaendelea kuwa vya kihuni na visivyo vya kiungwana, vita vina kanuni zake, lakini Trump huyu si mtu anayefuata kanuni.

Akieleza kwamba watoto 168 wa shule walikuwa wamefanya kosa gani, alisema: Katika sheria zote za dunia, watoto wanalindwa na hawapaswi kulengwa. Lakini maadui wanaigeuza sherehe ya harusi ya wananchi kuwa maombolezo. Kwa hiyo, kila mtu amethibitikiwa kwamba vita hivi ni vya kihuni na visivyo vya kiungwana. Hata hivyo, vikosi vyetu vya ulinzi na usalama vinajibu vita hivi vya kihuni kwa namna ya hali ya juu kabisa na kwa uungwana mkubwa.

Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran alisema: Kuna vita vya kijeshi, na vikosi vyetu vya ulinzi na usalama viko tayari. Adui anafanya shambulizi moja na anapokea majibu kadhaa, na majibu hayo yanatolewa; kwa hiyo tunajivunia vikosi hivi vya ulinzi na usalama.

Alisisitiza: Sambamba na vita vya kijeshi, kuna pia vita vya kiuchumi. Tangu mwanzo wa vita, au hata tangu mwanzo wa ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, maadui walikuwa wameanzisha vita hivi, pia kuna vita vya vyombo vya habari na kueneza uongo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, pamoja na vita vya kiutamaduni dhidi ya mfumo huu. Moja ya nyanja hizo ni vita vya kiuchumi, na tunapaswa kufanya jambo lile lile alilolifanya Mtume Mtukufu (saww).

Alikumbusha: Ninawaambia ninyi Umma ambao mliijaza mitaa kwa takribani siku 190 na zaidi ya miezi sita, kwamba msaada wenu kwenye mfumo wa Kiislamu katika uwanja huu ni muhimu. Viongozi wa mfumo wa Kiislamu wanapaswa kujitahidi kwa juhudi za kijihadi kutatua au kupunguza matatizo ya kiuchumi; ni haki ya wananchi hawa kwamba viongozi wafanye kazi kwa namna hii. Wananchi nao wanapaswa kufanya kila walicho nacho katika uwezo wao ili kuusaidia mfumo wa Kiislamu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha